
Khadija Omari Kopa huenda lisiwe jina geni sana kulisikia masikioni kwako, umaarufu ambao amejizolea kutokana na aina ya utunzi wa nyimbo anazozifanya(taarabu) Bi Khadija Omari Kopa ambae ni mzazi wa msanii Zuhura Omari Kopa maarufu kama (Zuchu). Leo hii ametembelea banda la JATU na kujifunza vitu vingi zaidi kuhusiana na JATU. Kubwa zaidi ni kuhusiana na BUKU TANO INATOSHA ambapo afisa masoko kutoka JATU walimueleza faida za kuwekeza katika hisa za JATU. Bila kusahau faida za kufanya kilimo chini ya usimamizi wa JATU.
Mara baada ya kupata elimu Bi Khadija aliwasihi vijana kuchangamkia zaidi fursa hii ya hisa kutokana na bei yake kuwa nafuu hivyo kila kijana mwenye uwezo wa kumiliki elfu tano(BUKU TANO) anaweza kuwa sehemu ya umiliki wa kampuni.
Jatu Talk Tv walipata nafasi ya kufanya mahojiano na balozi huyu wa JATU,unaweza kutazama kupitia youtube channel ya JATU TALK TV.
Mashaallah Bi Khadija ahsante sana kwakuwahamasisha vijana kukamata FURSA ya kununua Hisa JATU !! Wenye Akili watalifanyia kazi kadiri ya uwezo waliojaaliwa na Allah.
LikeLike