Kampuni ya JATU PLC ni miongoni mwa makampuni yanayoshiriki katika maonesho ya tano(5) ya bidhaa za viwanda yaliyoanza rasmi tarehe 3-9 Desemba 2020 chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara kupitia tasisi yake ya Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara ya Tanzania (TanTrade).
Maonesho haya ambayo yanafanyika katika Viwanja vya maonesho ya Sabasaba wilayani Temeke yanalenga kutambua mchango wa viwanda nchini na kujenga jukwaa kwa wadau wa sekta ya viwanda kupata fursa ya kubadilishana uzoefu na kutangaza fursa zinazopatikana katika sekta hiyo.
Kupitia maonesho haya, JATU PLC inapenda kuwakaribisha Watanzania wote kushiriki katika maoenesho haya na kuweza kujifunza fursa mbalimbali ndani ya JATU ikiwemo uuzwaji wa bidhaa za JATU zinazochakatwa katika viwanda vya JATU ikiwemo bidhaa za chakula kama maharage, mchele, unga wa lishe, sembe na dona, mafuta ya kupikia nk, shughuli ambayo inamuhakikishia mteja bidhaa ambazo zitamjengea afya bora na kumuongezea kipato kwa kupata gawio la faida kila mwisho kutokana na manunuzi ya bidhaa za JATU.
Akizungumza hivi karibuni katika maonesho hayo Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade Bi. Latifa Khamis amesema, “maonesho haya yanahamasisha Watanzania kutumia bidhaa zao kama kauli mbiu inavyosema, ‘Tumia bidhaa za Tanzania, Jenga Tanzania’‘, alisema Bi. LATIFA.




Hongereni Sana JATU kwakupiga hatua. Mungu yupo nanyi. Inshaallah.
LikeLike
habari. ni kipindi gani mnaanza kuandaa mashamba…. na jinsi ya kujiunga na jatu ni hatua gani nahitajika nizifanye_… nahitaji kukodi shamba hapo..
LikeLike
habari, tafadhali pakua app ya JATU inayopatikana playstore/appstore kisha jisajili n baada ya kukamilisha usajili na kufanya malipo ya kiingilio tsh 30,000/= utapokea ujumb kutoka JATU wenye namba yako ya uanachama pamoja na neno lako la siri, taarifa ambazo utakua ukizitumia kuingia kwenye app ya JATU na kupata taarifa mbalimbali. PIA WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA 0758396767 KUWZA KUPATA MAELEKEZO YA NAMNA YA KUKODI SHAMBA
ASANTE
LikeLike
Hi
LikeLike
HABARI, KARIBU JATU PLC
LikeLike