Habari,
Tungependa kuwajulisha wakulima wote wanaoshiriki kilimo cha mpunga na JATU Mbingu kuwa maendeleo ya mashamba yetu yapo vizuri, mpunga wetu umeshachanua na kwasasa tumefikia hatua ya palizi kwa awamu ya pili. Timu yetu ya wataalamu wa kilimo wanaendelea na zoezi la kukagua mazao ili kuhakikisha hayaathiriwi na magonjwa au wadudu.
Mvua zinazoendelea kunyesha pia zimekua neema kwetu kwani zao la mpunga linahitaji maji ya kutosha hivyo kupelekea mazao kukua kwa kasi. Tunategemea mpaka ifikapo mwezi June tutaanza kuvuna na kunufaika na uwekezaji wetu. Kilimo cha kisasa na chenye tija kisicho na usumbufu kinapatikana JATU pekee hivyo tunawahimiza watanzania kujiunga nasi tushirikiane kuboresha sekta ya kilimo, viwanda na masoko nchini.
Yaani napata faraja sana kuona nilichowekeza kwenye Jatu kikiendelea vyema….hongera uongozi wetu na Mungu atusaidie tuvune kama matarajio yetu.
LikeLike
Shukrani sana kwa kutuamini na kuwekeza nasi tutegemee mavuno mazuri msimu huu wa kilimo cha mpunga, pamoja tunaweza kufikia mafanikio tuliojiwekea
LikeLike