Jatu inapenda kuwataarifu wanachama wake kuwa tupo katika maonesho ya bidhaa zinazozalishwa na viwanda vya Tanzania, maonesho ambayo yanafanyika katika viwanja vya sabasaba maonesho barabara ya Kilwa.
Maonesho haya yameanza rasmi leo tarehe 05.12.2019 na kilele chake itakuwa ni tarehe 09.12.2019 Banda la Jatu ni namba 32 wote mnakaribishwa kujifunza fursa mbalimbali za Jatu na kujipatia bidhaa bora zinazoandaliwa na viwanda vya Jatu pamoja na huduma kuhusu Jatu Sacoss.