Katika muendelezo wa semina za JATU mtaa kwa mtaa kwa Dar es salaam na mikoani, leo tulipata wasaha wa kufanya semina kwa wakazi wa Manzese mtaa wa muungano ambapo wananchi mbalimbali walipata kuifahamu vyema JATU na fursa zake kupitia kilimo, viwanda, mikopo na masoko. Semina ya leo imehudhuliwa na vikundi mbalimbali vya kijamii ambapo wengi wameipenda JATU na kuahidi kuitumia hii fursa kujenga afya zao na kutokomeza umasikini.
JATU inaamini kuwa kama watanzania tukiungana na kuamua kuwekeza na JATU basi umoja wetu ndio chachu ya maendeleo yetu, hivyo kuwataka wananchi hao kufanya maamuzi sahihi kwa kuwa sehemu ya wanajatu. Fursa zilizopo ni nyingi hasa kwenye kilimo cha pamoja kisicho na stress, mikopo isio na riba pamoja na kula ulipwe ambapo huduma zote hizi zimelenga kutokomeza umasikini kwenye jamii zetu. Pia wakazi hao wamefurahishwa na uamuzi wa JATU kuelekea soko la hisa kwani utasaidia watanzania wote popote walipo kuweza kuwekeza kwenye hisa za JATU waweze kunufaika na magawio ya kila mwaka na faida nyingine ndani ya JATU.
JATU ni fursa ya watanzania wote
Wekeza na JATU kwa faida ya maisha yako
Jenga afya tokomeza umasikini